Thursday, May 17, 2012

THE STORY CONTINUES
Baada ya kuwa na ufahamu kuhusiana na hali yangu niliamua kuwa nataka nisome ili nije kuwa daktari ama nijitibu mwenyewe au nisaidie wenye matatizo kama yangu, na kama wengi wetu tujuavyo masomo ya sayansi huwa yanahitaji umakini mkubwa lakini kwa kuwa nilikuwa nikiumwa mara kwa mara na kulazwa mara nyingi nilijikuta nikiachwa nyuma kimasomo lakini kilichokuwa kikinisaidia ni kwa kuwa mungu alinipa akili za kuzaliwa zilizokuwa zikinisaidia katika masomo yangu na kunifanya nifanye vizuri mara kwa mara lakini hali ilibadilika nilipomaliza kidato cha pili na kusubiri matokeo, matokeo yalitoka na kwa bahati mbaya sikuwa nimefanya vizuri sana kwenye masomo ya sayansi hali iliyosababisha kuyeyusha ndoto zangu za kuwa daktari kwa maana ndo nilipeana mkono wa kwaheri na masomo ya sayansi, siku ile nililia sana kuona ndoto zangu zikiyeyuka mbele ya macho yangu pasi na kuwa na uwezo wa kufanya chochote ili kuzinusuru nililia hadi nafika nyumbani na nilipofika tu nyumbani nilianza kuumwa, nilikata mwezi mzima nikiwa kitandani hali ilikuwa mbaya sana maumivu yalikuwa makali sana, lakini nilipopata tu nafuu kitu cha kwanza ilikuwa ni kukimbilia ofisini kwa mwalimu mkuu kuomba huku nikilia wanifikirie mara mbili kwani sikuwa tayari kuona ndoto zangu zikiyeyuka……………….

JE, UNATAKA KUJUA KILICHOTOKEA NDANI YA OFISI YA MWALIMU MKUU?
UNATAKA KUJUA JIBU ALILONIPA? BASI TAFADHALI UNGANA NAMI SEHEMU IJAYO




After being aware about my health I decided that I want to study hard so I can be a doctor either to cure myself or atleast to help people with sickle cell like me, and as we all know science subjects are hard and they need a lot of concentration but because I was falling sick every now and then and being hospitalized many times I found myself behind my classmates in studies, what have been helping me is the nature of brain I had (common sense), god gave me common sense which helped me in my studies and made me do well most of the time but things got complicated when I finished form two and waits for results, when the results where out i realized that I didn’t do well in science subjects therefore my dreams went in vain because I had to say goodbye to science subject and enter in arts class for form 3 and 4. I cried a lot that day to see my dreams melted just like an ice infront of my eyes and couldn’t nothing to prevent that, I cried all my way going home and too bad when I reached home I got sick, a month passed by while I was still sick in bed my condition was really bad and the pain was unbearable. But when I got well the first thing to do was running straight to headmistress office crying to request them think about my situation twice because I wasn’t ready to see my dreams disappearing like that……..
DO YOU WANNA KNOW WHAT HAPPENED IN HEADMISTRESS OFFICE?
WHAT WAS HER REPLY? THEN JOIN ME IN THE NEXT EPISODE………..

0 comments:

Post a Comment