Thursday, May 24, 2012

TUENDELEE...

Ikabaki tu kusubiri uchaguzi wa shule utangazwe na kama nilivyodhamiria nilichaguliwa kujiunga na kidato cha tano katika shule ya sekondari Morogoro maarufu kama Moro sec mjini Morogoro. Kwangu binafsi nilifurahi kwa kuwa nilikuwa nimetimiza lengo langu lakini kwa wazazi wangu ilikuwa ni wasiwasi tele na mama alijaribu kunishawishi ili nikubali kufanya mpango wa kuhama shule lakini alikumbana na maswali ambayo hata yeye yalimfanya afikiri mara mbili na kwa shingo upande alikubaliana na maamuzi yangu nilimuuliza “Mama leo mko hai sawa, lakini kumbuka sisi ni wanadamu kuna leo na kesho, itakuaje mtakapofunga macho? Nitaishi na nani? Itanibidi nijifunze kuishi mwenyewe.”


So I stayed at home while waiting for the school selection to be announced and as I intended I was selected to join form 5 at morogoro secondary school well known as Moro sec. at morogoro region. I was more than happy because I fullfiled my goal but to my parents side it was fear and mom tried to convice me so that I can accept to shift to other day school but she met with questions that made her think twice and she accepted my decisions without full consent, I asked her “mom today you are alive, but remember we are human beings no one knows tomorrow, what will happen if you pass away? Who will I live with? I have to learn to live by my own and to take care of myself.”

0 comments:

Post a Comment