Tuesday, June 12, 2012

AFTER I COMPLETED FORM SIX

Wakati nilipomaliza kidato cha sita nilirudi nyumbani kama ilivyo ada na kama ilivyo kawaida huwa tunakaa muda mrefu tukisubiri matokeo hivyo nilikuwa tu nyumbani, na kama ilivyo kwa binadamu hasa vijana, msichana kama mimi ambaye kwa wakati huo nilikuwa binti mkubwa mapenzi hutokea wakati wowote pasi kutarajia. Basi kuna kijana pale mtaani akatokea kunipenda sana lakini baada ya kufahamiana kwa muda nilimwambia kuhusu hali yangu ya kiafya na akakubaliana nayo, baada ya muda kuna mtu pale mtaani alienda ofisini kwao na kumwambia mama yake kuwa “Namuona kijana wako akimfuata sana binti mmoja pale mtaani nikaona niwatahadhirishe kuwa Yule binti sio mzima ni mgonjwa na kifafa” akaenda na vielelezo ambavyo kwa kweli sijui alivitoa wapi na mpaka leo sijui ni nani kwa kuwa Yule kaka hakupenda kunitajia huyo mtu ila alinambia tu khadija kuwa makini na majirani sio wote wazuri wengine hawakutakii mema basi tangu hapo familia ya Yule kijana ikatokea kunichukia sanaaaa huku wakimshawishi kuachana na mimi japo aliwaelewesha kuwa siumwi kifafa na nilishamwambia kuhusu hali yangu na yeye alikubaliana nalo lakini walisisitiza kuwa hata kama si kifafa lakini hapaswi kuwa na binti mgonjwa kama mimi lakini namshukuru Mungu Yule kijana alikuwa muelewa aliendelea na msimamo wake na hata nilipokuwa naumwa alikuja hadi hospitali kuniona kuhakikisha nakula na kuhakikisha Napata matunda, maziwa na lishe nzuri. Alipata matatizo mengi sana kutoka katika familia yake kwa ajili yangu na mwisho wa siku maneno ya watu yakafanikiwa kututenganisha lakini namkumbuka hadi leo na katu sitomsahau kwa kuwa sijawahi kupendwa kama alivyokuwa akinipenda Yule kijana, nilichojifunza kutokana na hili ni kuwa unyanyapaa katika jamii kwa watu wenye hali kama yangu ya kiafya upo tena sana tu hatukubaliki katika jamii tunatengwa kitu ambacho binafsi kiliniumiza sana nikatamani nibadili nilivyo niwe mtu mwengine lakini ni jambo ambalo halikuwezekana na halitawezekana.


When I completed form six I came back home as we all do and as we all know that we spent much time waiting for the results so I stayed at home, and as it is to human beings especially youth, a girl like me who at that time was a teeneger love happens anytime without expecting. There was a boy in our street who fell very much in love with me but after some time of knowing each other I told him about my health condition and he accepted it, after sometime since I told him about my condition someone from our street went to his parents and told them that their son is seeing me and that he/she wanted to alert them because iam not well im suffering from fits and that person went with documents evidence that I didnt know where he/she got it and I also don’t know who it was because when that guy told me he didnt want to say who was it , all he said was I should be careful because not everyone loves me others dnt wish me well so since then that boy’s family happen to hate me so much and convinced him to forget about me because they don’t need me in their family though he explained to them that im not suffering from that disease and that he knows because I have told him about my condition and he is ready to be with me but they insist that even if it is not fits, its not proper for him to be with sick girl like me but I thank god the guy was very understanding and very stable with his decisions and when I was sick he was always at the hospital making sure that I eat and get fruits, milk and balanced diet. He went through many problems from his family because of me and at the end of the day rumors and gossips succeeds to separate us but I still remember him until today and I will never forget him because I have never been loved the way he did, what I learnt from this event is that there is isolation of people like me in our society especially African societies, this awareness hurt me so much that I wished I could change the way I was and became another person but its something that was not possible and will never be.

0 comments:

Post a Comment