Monday, June 11, 2012

LIFE AT MORO SEC

Ilifika wakati mwengine ilimbidi mama kupanda gari hadi Mororgoro kunichukua nyumbani kwa mmoja wa kaka zangu na kuniuguza hadi nipatapo nafuu ndo huondoka na kurejea ofisini hayo ndo maisha yangu nillipokuwa moro sec. wakati nikiwa kidato cha sita nilianza kuhisi hali tofauti katika mwili wangu hasa ilipofika usiku wa manane, nilihisi tumbo likiniwaka moto mara kwa mara niliamka na kuhangaika kutafuta chochote kitakachonipa nafuu baadae hali ilizidi ikanibidi nirudi nyumbani na baada ya vipimo nikagundulika kuwa na vidonda vya tumbo tatizo jengine likanipata. Kwa kweli hadi leo bado sijang’amua hali iliyosababisha kupata tatizo hilo lakini hadi sasa ninalo na huwa ninateseka mara mbili pale ninapoumwa.
Jambo jingine lilokuwa likinitesa nilipokuwa Moro sec ni mwalimu wangu wa darasa, mwalimu Yule alikuwa akinichukia na chuki yake ilidhihirika wazi machoni bila kificho na kwa kweli hadi leo sikujua sababu labda kwasababu nilikuwa mgonjwa na hakuweza kunipiga kila alipoamua kuchapa darasa zima, kwa maana alikuwa na tabia ya kuchapa darasa zima akikuta makelele darasani na kila mara alikuwa akiongea maneno ya kejeli kabla ya kuanza kuchapa utamsikia “Mi nakung’uta wote sijali nani ana mashetani wala nani ana nini, we kama una mashetani pandisha” kisha darasa zima huanguka kicheko pia kila alipokuwa akifikia nilipokuwa nakaa mimi kwa kuwa karibu darasa zima walikuwa wananijua naumwa hawakusita kusema “Mwalimu huyo hachapwi anaumwa” na yeye hujibu anaumwa nini? Nyie ndo madaktari au mashabiki wake mi nampiga na vitu vya namna hiyo. Darasani tulikuwa wagonjwa wawili Mimi na kuna msichana mwengine ambaye alikuwa akianguka mara kwa mara akipigwa, kwa kweli mwalimu huyu alinipa wakati mgumu sana mpaka namaliza moro sec lakini namshukuru Mungu nilimaliza kwa amani.

It reached a time that my mother had to come to morogoro and take me to one of my brothers house and take care of me until I get better then she leave and go back to office, that’s how my life was when I was in moro sec. when I entered form six I started feeling something different in my body especially in midnight, I felt something like fire in my stomach, I would woke up and found anything that would make me feel better then later the condition got worse so I had to go back home and after some tastes It was found that I develop some ulcers in my stomach, another problem was born. Until today I haven’t been able to know what caused it but I have it until now and when I get sick I suffer twice.
Another thing that made me suffer when I was at Moro sec was my class teacher, oh my! The teacher hated me so much and she couldn’t even hide it, it was very clear in her eyes, until today I don’t know why she hated me that way was it because I was sick and she couldn’t beat me whenever she decide to beat the whole class, because she had the habit of beating the whole class whenever she find people making noise in the class without asking who was making noise and who wasn’t and everytime she does that she was speaking insults before doing that you will hear her “I beat all I don’t care who has evil spirits or who has what, if you have spirits then let them show theirselves” then the whole class would start laughing, also when she was getting near where I was sitting because almost the whole class knew that I was sick so they always said “teacher she is sick you cant beat her” the she would reply “what is she suffering from? Are you the doctors or just her fans, iam going to beat her and other things like that. In our class we were two sufferers, I and another girl who was falling constantly whe she was beaten, frankly she gave me a hard time studying there until I completed but I thank god that I completed peacefully.

0 comments:

Post a Comment