Saturday, June 23, 2012

UNPLEASANT SITUATIONS CONTINUES...

Pia wakati nipo chuoni mwaka wa kwanza nilichaguliwa kuwa kiongozi wa darasa na mara nyingi nilikuwa nikienda ofisini kwa walimu kwa kuwa nilikuwa kiunganishi kati ya walimu na wanafunzi wa darasa langu na watu wa sickle cell tuna utambulisho wetu si mara zote lakini mara nyingi tunapokuwa katika crisis (kipindi cha mvunjiko wa seli) macho hubadilika rangi na kuwa ya njano tofauti na binadamu wa kawaida ambao macho yao huwa meupe, kwa kweli hilo nalo pia limekuwa ni changamoto kwangu maana limekua likizua maswali mengi sana kwa watu na limekuwa likininyima uhuru na kujiamini pindi niwapo mbele ya macho ya watu katika kipindi hicho na kwa kuwa wengi hawajui hujikuta wakinidhihaki mara kwa mara na pia limekuwa likinifanya niulizwe maswali mengi sana kila nilipokua niendapo ofisini kwa walimu lakini ilibidi nijifunze kuikubali hali lakini jingine ambalo nilikumbana nalo ni hasira, jambo ambalo nahisi limewahi kunigombanisha na watu wengi sana bila mwenyewe kujijua lakini kama ilitokea nikamkwaza mtu yeyote kwa ajili hiyo leo namuomba msamaha mbele ya watu wote mnaosoma makala hii sasa hivi. Hii hali hunikuta mara kwa mara nina hasira za haraka na huwa mtihani sana kutoweka na nilipojaribu kufuatilia nakumbuka siku moja wazazi wetu na sisi tulipokuwa tukipatiwa elimu juu ya watu wenye matatizo haya waliwahi kuambiwa wawe wavumilivu sana katika kutulea maana wagonjwa wa sickle cell huwa na hasira sana mara kwa mara hivyo la muhimu ilikuwa ni kutuelewa na kutukubali. Lakini pia namshukuru Mungu, kwani kwa sasa najitahidi sana kuidhibiti hali hii na nashukuru Mungu kuna mabadiliko makubwa si kama zamani.


Also when I was at the university first year I was selected as a class representative and I was going to lecturer’s offices constantly because I was a medium between teachers and students of my class and sickler people have their identity though its not all the time but most of the time when we are in crisis (when the cells breaks) our eyes become yellowish different from normal human beings who theirs eyes are always white, this has also been a challenge to me because it has been rising lots of questions to people and has been denying me the freedom and confidence whenever iam infront of people’s eyes, while others have been mocking me because they didn’t know what was wrong with me, it made me to be questioned alot whenever I went to the stuff offices but I had to learn to accept my condition. Also another challenge was anger, something that I think provoked me to fight with so many people without me noticing but if it has ever happened that i hurt anyone in one way or another, today I take this opportunity to ask for forgiveness infront of everyone who is reading this article right now. This situation happens to me constantly I usually get angry fast and it takes time to go away, so I decided to do some follow ups why it is like that and I remembered one day when we were at the clinic getting some training about people with sickle cell our parents and us were once told that they should be very patients living with us because we have tempers so its important to accept and understands us. But I also thank god, because now im really doing my best to prevent that condition and thank god I can see some improvement comparison with the beginning.

0 comments:

Post a Comment