Saturday, June 2, 2012

sorry kwa kuchukua muda mrefu kupost muendelezo wa story lets continue

Kwa siku za mwanzo maisha yalikuwa mepesi na ya kawaida lakini hali ilikuwa tete pale nilipoanza kuumwa na hii ilitokana na kupata malaria mara kwa mara ugonjwa ambao ni adui yangu mkubwa na ndo ugonjwa ambao huamsha yote yaliyolala. Kwa kweli nilipoumwa nilipata tabu sanaaaa kwa kuwa kwanza ilikuwa ni lazima nilazwe hospitali ya mkoa kwani nilikuwa ni mwanafunzi wa shule ya serikali, na kama tujuavyo hospitali nyingi za serikali huwa na huduma mbovu na duni na kutokana na hali yangu nilihitaji uangalizi wa ziada hapo ndipo nilipokuwa nikikumbuka wazazi, nikatamani ningekuwepo nyumbani au hata mama yangu angekuwa karibu yangu, nilikatwazwa kulala na mtu yeyote marafiki zangu walikuwa wakifukuzwa na hivyo kulazimika kulala peke yangu, na nilipokuwa nikizidiwa na kulalama kwa maumivu usiku hakuna aliyekuwa akijali wala kushtuka sana sana labda unakuwa umewapatia la kuongea wakati wa kukabidhiana zamu utawasikia “Huyu ana ni sickler vikimzidia utamuona anajipinduapindua tu kitandani, kisha wote wanaangua vicheko” hizo ndo huduma za hospitali zetu za serikali. Vyoo pia vilikuwa vichafu mno muda mwengine hata maji hakuna hivyo kuoga ilikuwa ndoto za abunuasi, pili nilipokuwa moro sec mara nyingi nilipokuwa nikizidiwa usiku kama kawaida ilinibidi kuvumilia hadi asubuhi na pengine bado inapofika asubuhi matron akifuatwa atajibu anasali tumsubiri hadi amalize kusali ikiwa mimi naumia mana maumivu ya sickle cell huwa makali sana kiasi cha muda mwengine kupatwa na ganzi ya viungo hasa meno pamoja na hayo yote nawashukuru sana watu ambao walikuwa nami siku zote za kuumwa kwangu nitawashukuru hadi pumzi yangu ya mwisho MWANAHAWA, MELANIA, KALISTA, JULIE, SUBIRA na FAITH, FINA, EVE, na yeyote ambaye nimemsahau lakini unajua kwa njia moja ama nyingine ulinisaidia natumia fursa hii kukushukuru for everything.

In early days life was very simple and normal but things got complicated when I started falling sick and this was because of getting malaria every now and then, the disease which is my greatest enemy and which cause worsening of my condition. Honestly when I fall sick I was in bad shape because first I had to be admitted in government hospital since I was a government student, and as we all know most of government hospitals have poor services and because of my condition I needed an extra care and that’s what reminded me of my parents, and wish I was home or even my mother would have been there with me, I wasn’t allowed to sleep with anyone and when my condition get worse because of the pain at night nobody cared, you will just give things to say when they exchange the turns at morning “she is sickler when the pain become unbearable you will see her twisting herself from one side of the bed to another, and they all laugh” those are the services of our government hospitals. Toilets were also too dirty and without water so to have bath was not possible sometimes, second when I was in mororgoro secondary and my condition got worse at night I had to be patient until morning and even so when the morning come and when they go to tell matron, she will say that she is praying so we have to wait until she finishes while I was hurting because the sickle cell pain is very painfull and hard to handle and sometimes leading to numbness of muscles and teeth but above all that I would like to thank some people who were always with me when I was sick always supporting me as follows; MWANAHAWA, MELANIA, KALISTA, JULIE, SUBIRA, FAITH, FINA, EVE and whoMever I ddnt mention but you know you helped me in one way or another I take this opportunity to thank you for everything.

0 comments:

Post a Comment